1. Ee Mungu twaomba uilinde

Jumuiya Afrika Mashariki

Tuwezeshe kuishi kwa amani

Tutimize na malengo yetu.

 

Chorus

Jumuiya Yetu sote tuilinde

Tuwajibike tuimarike

Umoja wetu ni nguzo yetu

Idumu Jumuiya yetu.

 

2. Uzalendo pia mshikamano

Viwe msingi wa Umoja wetu

Natulinde Uhuru na Amani

Mila zetu na desturi zetu.

 

3. Viwandani na hata mashambani

Tufanye kazi sote kwa makini

Tujitoe kwa hali na mali

Tuijenge Jumuiya bora.